Kampuni
ya Ulinzi ya G1 Ltd leo imeunga mkono Juhudi za serikali ya Mkoa wa Dar es
salaam katika Mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona kwa kutoa Generator moja
kwaajili ya kuzalisha umeme kwenye Vituo vilivyotengwa kwaajili ya tatizo la
Corona kama ikitokea dharura ya umeme ukikatika.
Akipokea
Mchango huo kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda,
Mganga mkuu wa Mkoa huo Dr. Rashid Mfaume ameishukuru Kampuni hiyo kwa kuunga
mkono juhudi za serikali ambapo ameeleza licha ya kutoa Generator hiyo pia
walitoa Ambulance moja ambayo inaendelea kutoa huduma kwenye Hospital ya
Mloganzila.
Kwa
upande wake Afisa rasilimali watu wa Kampuni ya G1 Security Ltd Bw. Seleman
Yusuph amesema Kampuni hiyo itaendelea kushirikiana ofisi ya Mkoa katika
masuala mbalimbali ya kijamii.
No comments:
Post a Comment