Polisi Ruvuma wataka wananchi wafichue wahalifu - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, April 1, 2020

Polisi Ruvuma wataka wananchi wafichue wahalifu


Na Amon Mtega –Songea

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Simon Maigwa, amewataka wakazi wa mkoa huo kutoa taarifa za watu wanaofanya vitendo viovu kwenye jamii ili kuvikomesha.

Wito huo aliutoa jana wakati akionyesha baadhi ya vitu vilivyoibwa kwa wananchi, zikiwemo televisheni, mafuta ya kula, pombe na spika za redio vilivyokamatwa kwenye msako unaoendelea mkoani hapa.

Kamanda Maigwa alisema ili kukomesha vitendo hivyo, wananchi wanatakiwa kuimarisha ulinzi na kuendelea kutoa taarifa za watu wanaovifanya.

Alisema kufuatia uhalifu huo watu wanne wanashikiliwa na polisi na upelelezi wa kuwabaini wengine unaendelea ili kuuvunja mtandao wa wahalifu.

Kamanda Maigwa alisema wahalifu hao wamekuwa wakivunja majumba ya watu na maduka kisha kuiba mali zikiwemo televisheni.

Alisema baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria ili wajibu tuhuma zinazowakabili.

Kamanda Maigwa aliwataka wakazi wa mkoa huo ambao waliibiwa vitu vyao, kwenda kuvitambua vitu Kituo Kikuu cha Polisi.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages