Mhariri wa magazeti ya New Habari 2006 Ltd Bakari Kimwanga akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania Udiwani Kata ya Makurumla wilayani Ubungo jijini Dar es Salaam na Katibu CCM Kata ya Makurumla Salama Mlaponi(kulia). Kimwanga amechukua fomu hiyo leo Julai 15, 2020
Katibu wa CCM Kata ya Makurumla wilayani Ubungo jijini Dar es Salaam (kulia) akijaza risiti ya malipo ya fomu ya udiwani ambayo yamelipwa na Kada wa Chama hicho Bakari Kimwanga.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Bakari Kimwanga akiwa ameshika fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Udiwani Kata ya Makurumla
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Angel Akilimali akiwa ameshika fomu ya kuomba ridhaa ndani ya Chama chake kuwania Ubunge Jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam.
Angell Akilimali (wa pili kulia) akiwa na baadhi ya wanachama wa CCM ambao wamefika Ofisi za Chama hicho wilaya ya Ilala baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge jimbo la Ukonga.
No comments:
Post a Comment