Baba wa Nicki Minaj afariki kwa ajali ya gari - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Monday, February 15, 2021

Baba wa Nicki Minaj afariki kwa ajali ya gari


Baba wa mwanamuziki wa miondoko ya kufokafoka, Nicki Minaj, 64, ameaga dunia baada ya kugongwa na gari kisha dereva kukimbia mjini New York, polisi wameeleza.

Robert Miraj alikuwa akitembea kando kando ya barabara katika kisiwa cha Long siku ya Ijumaa na kugongwa na gari, kisha dereva wa gari hiyo aliendelea na safari, polisi katika kaunti ya Nassau imesema.

Miraj alipelekwa hospitalini ambako alithibitishwa kufariki siku ya Jumamosi.

Polisi wametaka shuhuda yeyote wa tukio hilo baya kujitokeza. Gazeti la the Guardian limeripoti .

Minaj, 38, kwa jina Onika Tanya Miraj alizaliwa huko Trinidad na alikulia jijini New York City borough of Queens.

Mwanamuziki huyo hajajitokeza kuzungumza chochote kuhusu kifo cha baba yake.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages