MAKAMPUNI SITA YAAHIDI KUTOTENGENEZA MAGARI YA MAFUTA IFIKAPO 2040 - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, November 10, 2021

MAKAMPUNI SITA YAAHIDI KUTOTENGENEZA MAGARI YA MAFUTA IFIKAPO 2040

Makampuni sita ya magari yameahidi kuacha kutengeneza magari yanayotumia mafuta ifikapo mwaka 2040, kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kupunguza uzalishaji wa gesi chafu.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na serikali ya Uingereza ambayo ndio mwenyeji wa mkutano wa Tabianchi wa COP26.

Lakini duru zinazohusika na makubaliano hayo zimesema makampuni mawili makubwa ya magari ya Toyota na Volkswagen hayakusaini makubaliano hayo.

Aidha kampuni ya Sweden ya Volvo imesema inajiandaa kutengeneza magari yanayotumia umeme tu ifikapo mwaka 2030.

Uingereza, imesema nchi nyingine nne zikiwemo New Zealand na Poland zimejiunga na mataifa ambayo tayari yamejitolea kuhakikisha magari yote mpya yatakuwa hayatoi gesi chafu hewani ifikapo mwaka 2040.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages