
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla leo ameshiriki katika Mkutano wa Saba wa Baraza la Kumi la Wawakilishi.
Katika Kikao hicho Mhe. Hemed ambae pia ni Mtendaji Mkuu wa Shughuli za Serikali katika Baraza la Wawakilishi ameshuhudia uwasilishaji wa Hotuba Bajeti Kuu ya Serikali iliyowasilishwa na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Sada Mkuya Salum.

Aidha Mhe. Hemed ameambatana na Mkewe Mama Sharifa Omar Khalfan katika Tafrija fupi iliyoandaliwa baada ya kukamilika kwa Uwasilishaji wa Hotuba hiyo.



No comments:
Post a Comment