SMZ YAJIPANGA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Friday, June 10, 2022

SMZ YAJIPANGA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI

Serikali ya Mapinduzi ya zanzibar itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji ili kuja kuwekeza kwa kukuza pato la nchi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo Ofisini kwake Vuga alipokutana na wawekezaji kutoka nchi mbali mbali.

Mhe. Hemed ametumia fursa hiyo kuwakaribisha kuja kuwekeza katika sekta mbali mbali hasa sekta mama ya uchumi wa Buluu.

Aidha Mhe. Hemed ameeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji ikiwemo kuongeza idadi ya watalii nchini kupitia vivutio mbali mbali vilivyopo akigusia baadhi vilivyomo katika filamu ya Royal Tour.

Nae waziri wa Utalii na Mambo ya kale mhe Simai Moh'd Said amesema kuwa Zanzibar ina sehemu nyingi za uwekezaji hasa katika utalii kulingana na mazingira yake yaliyopo Nchini.
Amesema faida kubwa ya Zanzibar ni kuona kuwa wawekezaji wanaongezeka kwa wingi kuja kuwekeza na kueleza kuwa Wizara inaweka mazingira mazuri akitolea mfano kilimo cha Spice na kuboresha miundombimu hasa katika sekta ya Utalii.


No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages