BENKI YA ABSA YAJIZATITI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, March 18, 2026

BENKI YA ABSA YAJIZATITI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE

Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka, akitoa mada katika kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kulia), akipokea cheti cha shukrani kwa udhamini kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Acceleration Foundation, Bi. Bernice Fernandos, wakati wa Kongamanao la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja anayeshughulikia miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso, Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka, na Bi. Cygrade Othman pia kutoka benki hiyo.
Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka (katikati), na Bi. Munira Chambuso (kushoto) kutoka Absa, wakimsikiliza mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Dewji, wakati wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Bi. Thamrat Khamis (kushoto), anayeshughulikia akaunti za biashara ndogo na za kati (SME) akizungumza na mmoja wa washiriki wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Ukidhaminiwa na Benki ya Absa, mkutano huo uliwaleta pamoja viongozi wanawake kuchunguza namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyosukuma mustakabali wa taifa.
Wakishangilia, ni timu ya timu kutoka Benki ya Absa, ikiongozwa na Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya Kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Forum’ likifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo, liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages