
Kati ya hizo, tatu zilikuwa zinakaimiwa na mbili waliokuwa wakuu wa wilaya hizo uteuzi kutenguliwa.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Zena Said, Ali Abdalla Said Natepe ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharib B akichukua nafasi ya Amour Juma Mmanga ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo Natepe alikuwa Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mjini Magharibi. Riziki Daniel Yussuf ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A akichukua nafasi ya Rashid Simai Msaraka ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wengine walioteuliwa ni Dk Said Haji Mrisho anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja. Kabla ya uteuzi huo alikuwa katibu Tawala wa wilaya hiyo.
No comments:
Post a Comment