Dar es Salaam 18 Februari 2025: Kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Yas, pamoja na Samsung Tanzania zimezindua simu mpya aina ya S25 ambayo imekuja na teknolojia ya akili mnembayaani Artificial intelligence (AI).
Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha simu za mkononi wa Samsung, Mgope Kiwanga amesema wao kama Samsung wanayofuraha kutambulisha bidhaa hiyo hapa nchini ambapo kupitia simu hiyo Watanzania wataweza kuona mabadiliko makubwa kupitia simu hizo.
Aidha Mgope amesema mbali na toleo hilo la S25 pia kuna matoleo mengine mawaIi ambayo ni Samsung ultra na base ambapo kila moja litakuwa na waranti ya mwaka mmoja, ambapo kupitia ushirikiano huo na Yas mteja atapata mambo mazuri ikiwemo kupata GB96 kutoka Yas Tanzania, amesema Mgope.
Kwa upande wake Meneja Huduma za Ziada ya Yas, Bi.Ikunda Ngowi amesema wao kama Yas wanayofuraha kushirikiana na Samsung kupitia bidhaa zao ambapo wao kwa kunogesha uzinduzi huo wameamua kutoa GB 96 kwa mwaka
No comments:
Post a Comment