Katika Kujikinga na maambukizi ya virusi vya
ugonjwa wa Corona na kuepuka mikusanyiko , Kuanzia leo Aprili 13 mwaka 2020
Mikutano ya Waandishi wa Habari na shughuli nyengine zitakazowafanya waandishi
wa habari kukusanyika zinasitishwa.
Hivyo, basi taarifa za Waziri wa Afya Zanzibar
kuhusiana na Virusi vya ugonjwa wa Corona zitatolewa kwa njia ya 'Press
Releases', kurusha moja kwa moja kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC)
au kurekodiwa na kusambaza taarifa hiyo kwa vyombo vya habari na umma kwa ujumla.
Taasisi zote zenye shughuli zitakazowajumuisha
waandishi wa habari tunawaomba kutumia njia tulizozieleza na kujiepusha kwa
namna yoyote ile kuwaita waandishi wa habari katika shughuli zao.
Wahariri na waandishi wa habari tunawasisitiza
kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya na Serikali kwa ujumla kwa kuepuka
mikusanyiko Dkt Juma ohammed alum Mkurugenzi Idara ya Habari.
No comments:
Post a Comment