Mamlaka ya Usalama wa Anga nchini imefuta safari za ndege zote za abiria za kimataifa na kuweka vikwazo zaidi kwa ndege maalum za mizigo zitakazoruhusiwa kutua nchini. Hii ni hatua nyingine ya kupambana na Ugonjwa wa Covid-19.
Kwa
mujibu wa taarifa ya TCAA, safari zote za ndege zilizokuwa zimepangwa na zile
ambazo hazikuwa zimepangwa zimezuiwa hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.
Licha
ya zuio hilo, TCAA imebainisha kuwa ndege za mizigo zitaruhusiwa kuingia
nchini, lakini wahudumu wa ndege hizo watawekwa Karantini kwa gharama zao
katika maeneo yaliyotengwa na serikali kwa kipindi chote watakachokuwa nchini.
Mpaka
April 13, Tanzania immeripoti visa 46 vya maambukizi ya virusi vya Corona, vifo
vitatu na wagonjwa saba wamepona.
No comments:
Post a Comment