Na Dixon Busagaga, Moshi
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt Charles Kimei amejitokeza kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Vunjo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, hali inayoashiria uwepo wa mchuano mkali miongoni mwa makada wa Chama hicho waliojitokeza kuchukua fomu hii leo.
Ikumbukwe Jimbo la Vunjo limekuwa chini ya James Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR-Mageuzi Taifa.
No comments:
Post a Comment