
Henry Momanyi, Mmarekani mweusi wa asili ya Kenya, anagombea kiti cha udiwani katika mji wa Brooklyn Park, eneo wakilishi la West District, jimbo la Minnesota kwa tikiti ya chama cha Demokratik.
Momanyi, mwenye umri wa miaka 51, anagombea nafasi inayoshikiliwa na Diwani Susan Pha wa chama cha Republikan, anayewania tena katika uchaguzi wa mwaka huu utakaofanyika Jumanne tarehe tatu mwezi Novemba mwaka huu.
Wanasiasa hao wawili walishinda tikiti za vyama vyao kwenye uchaguzi wa awali na kuteuliuwa na vyama hivyo mapema mwaka huu.
Katika mahojiano na idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika, Momanyi amesema ana matumaini makubwa ya kupata ushindi kwa sababu amepata uungwaji mkono na wakazi wengi wa mji huo, wakiwa ni pamoja na wahamiaji kutoka bara la Afrika.
No comments:
Post a Comment