
Na Mwandishi wetu | DAR ES SALAAM | Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala Mhe Omary Kumbilamoto amefanya ziara yake ya kikazi katika Shule ya Secondary Mbondole ambayo imepandishwa hadhi kuwa Shule ya Wilaya.
Katika ziara hiyo Mhe. Meya aliambatana na Afisa Elimu Secondary Manispaa ya Ilala Mwal. Mussa Ally, Diwani wa Kata ya Msongola Mhe. Mwalile pamoja na Diwani wa Viti Maalum Mhe. Magdalena.
Aidha Mwalimu Mkuu huyo alimalizia kusoma taarifa yake kwa kumuomba Mstahiki Meya Kumbilamoto kukubali Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 120 yapewe jina lake ambapo Meya Kumbilamoto alikubali.
Akiongea katika hafla hiyo Mhe. Kumbilamoto licha ya kukubali Mabweni hayo kuitwa Jina lake alizipokea Changamoto zote zilizowasilishwa na Mkuu wa Shule hiyo nakuwasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kuzingatia masomo kwani Taifa linawategemea.
"Serikali inafanya mambo mengi katika kuboresha Sekta ya Elimu kwaajili yenu hivyo ni vyema kuzingatia Elimu kwani Taifa linawategemea sana" Alisema Kumbilamoto.
Chanzo, Pugu Online.


No comments:
Post a Comment