UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UKRAINE WATOA TAMKO, WANAODHANI KUKAA NCHINI HUMO SIO SALAMA WAONDOKE - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Thursday, February 24, 2022

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UKRAINE WATOA TAMKO, WANAODHANI KUKAA NCHINI HUMO SIO SALAMA WAONDOKE

UBALOZI wa Tanzania nchini Ukraine umetoa tamko kuhusiana na hali ya sintofahamu ya kiusalama inayoendelea nchini humo.

Taarifa iliyotole wa na Ubalozi wa Tanzania nchini humo, imeshauri kuwa wote wanaodhani kukaa Ukraine kwa sasa sio salama waondoke nchini humo.

Aidha kwa wazazi wenye watoto wanaosoma nchini humo na wanataka watoto wao warejee kwa muda hadi hapo uvumi wa kutokea vita utakapoisha, wafanye utaratibu binafsi wa kuwarudisha watoto wao nyumbani kwa kutumia ndege za abiria zinazofanya safari kutokea Ukraine.

Pia ubalozi umeshauri wanafunzi wanaotaka kurudi nyumbani wawasiliane na uongozi wa vyuo wanavyosoma na kukubalina kuendelea kwa masomo kwa njia ya mtandao (Online) kipindi chote watakachokuwa nje ya Ukraine.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages