SANAA: KITIME ATAHADHARISHA BENDI KUPIGA KWENYE BAR - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Tuesday, February 28, 2017

SANAA: KITIME ATAHADHARISHA BENDI KUPIGA KWENYE BAR


Wasanii na vikundi vinavyopiga muziki wa bendi wametakiwa kujitazama upya juu ya muziki huo kutumika kama chombo cha kuuzia bia kwenye Bar.

Hayo yamesemwa na msanii nguli wa muziki wa dansi hapa nchini John Kitime alipokuwa akizungumza na wasanii pamoja na waandishi wa habari katika jukwaa la sanaa lililoandaliwa na Baraza la Sanaa nchini (BASATA).

“kuna vitu tunafanya tunaona kama vya kawaida lakini ndio vinaua muziki wetu kama leo hii, bendi zinapiga kwenye bar kwa ajili ya kuuza bia na watu wanaangalia bure, hivyo inamaanisha bendi zetu ndio kichocheo cha kuuza pombe katika mabaa yote mjini” amesema Kitime.

Kitime ametoa wito kwa wasanii kuanza kubadilisha mtindo wa maisha kwani kitendo cha bendi zote kuhamia kwenye bar ni moja ya anguko kubwa la muziki wa dansi nchini.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages