ALI KIBA KUTIMKA KESHO MAREKANI, KUPIGA SHOO TANO - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, March 1, 2017

ALI KIBA KUTIMKA KESHO MAREKANI, KUPIGA SHOO TANO

Siku moja mara baada ya kuwasili nchini akiwa na tuzo ya MTV base msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba, ameondoka nchini kwenda Marekani kwa ajili ya maonyesho yake ya kimuziki katika nchi hiyo.

Akizungumza na mwandishi wa Wor'Out Media, mdogo wa msanii huyo Abdul Kiba amesema kuwa kiba amerudi nchini kwa ajili ya kuleta tuzo ya MTV kwa Watanzania na hivyo kesho jioni tunaondoka kwenda marekani.

“tunaondoka kwenda marekani na tutafanya maonyesho matano katika miji tofauti ya nchi hiyo hivyo mashabiki wetu waendele kutegemea kupata makubwa kutoka kwetu” amesema Abdul Kiba.

Amesema kuwa  kwa sasa ratiba yao ipo taiti katika kufanya maonyesho ya kimataifa na wakirejea watafanya kitu kikubwa kwa watanzania na Afrika kwa ujumla.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages