BENKI YA BARCLAYS TANZANIA LIMITED YAZINDUA UNION PAY - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Sunday, April 9, 2017

BENKI YA BARCLAYS TANZANIA LIMITED YAZINDUA UNION PAY


Aprili 06, 2017, Dar es Salaam, Tanzania

Benki ya Barclays Tanzania leo imezindua huduma ya Union Pay kama njia moja wapo ya kuwarahisishia wateja wenye kadi za Union Pay kufanya miamala na kutumia kadi zao wakiwa nchini.

Mkurugenzi Mtendaji, Abdi Mohamed amesema benki ya Barclays Tanzania imezindua huduma hii ambayo itatolewa kupitia mashine za ATM na POs zilizosambaa nchini.

Huduma hii ni nafasi kubwa kwa wafanya biashara wenye POs kwenye maduka, hoteli, migahawa, mbugani na kadhalika kuweza kuwahudumia na kufanya biashara wateja wenye kadi za Union Pay .

“Huduma ya Union Pay inapatikana nchi 160 duniani ambazo zinaongoza kwa kutembelewa na wachina kwa ajili ya biashara, kazi au starehe ikiwamo Tanzania hivyo tumeona fursa na haja ya kuanzisha huduma hii kwa wateja wenye kadi za Union Pay kupitia mashine zetu za ATM na POs.

Kwa mzunguko wa zaidi ya POs 500 na ATM 52 nchini, huduma hii itawasaidia wateja kwa kukidhi mahitaji yao kwa wakati na kama mpango mkuu kwa benki tutahakikisha inawafaidisha watumiaji wa Union Pay nchini na dunia nzima” alisema Abdi.

Union Pay International inayojulikana kama Union Pay ni huduma kuu ya kifedha inayopatikana kupitia kadi za kibenki na ina makao makuu yake mjini Shanghai, China.

Huduma hii imezinduliwa Machi 26, 2002 na inaendeshwa chini ya benki kuu ya China - People’s Bank of China (PBOC)  

Huduma hii pekee ndio inayounganisha mitandao yote ya mashine za ATM nchi nzima na pia ni mtandao wa EFTPOS (Electronic Funds Transfer at Point of Sale)

Mkuu wa Maendeleo ya Biashara wa Kadi ya Union Pay, Herman Botes (kushoto), akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki ya Barclays Tanzania kama njia moja wapo ya kuwarahisishia wateja wenye kadi hizo kufanya miamala na kutumia kadi zao wakiwa nchini kupitia benki hiyo. Uzinduzi umefanyika jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto kwake ni Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei, Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed, Mkurugenzi wa Huduma Rejareja na Biashara wa Barclays, Kumaran Parther na Meneja wa Kadi wa benki hiyo, Philbert Casmir.
Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki ya Barclays Tanzania kama njia moja wapo ya kuwarahisishia wateja wenye kadi hizo kufanya miamala na kutumia kadi zao wakiwa nchini kupitia benki hiyo. Uzinduzi umefanyika jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto kwake ni, Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed, Mkurugenzi wa Huduma Rejareja na Biashara wa Barclays, Kumaran Parther.
Mkurugenzi wa Huduma Rejareja na Biashara wa Barclays, Kumaran Parther akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay.
Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed, akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki ya Barclays Tanzania kama njia moja wapo ya kuwarahisishia wateja wenye kadi hizo kufanya miamala na kutumia kadi zao wakiwa nchini kupitia benki hiyo. Uzinduzi umefanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei, kulia ni Mkurugenzi wa Huduma Rejareja na Biashara wa Barclays, Kumaran Parther na Meneja wa Kadi wa benki hiyo, Philbert Casmir.

Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei, akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki ya Barclays Tanzania kama njia moja wapo ya kuwarahisishia wateja wenye kadi hizo kufanya miamala na kutumia kadi zao wakiwa nchini kupitia benki hiyo. Uzinduzi umefanyika jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto kwake ni Mkuu wa Maendeleo ya Biashara wa Kadi ya Union Pay, Herman Botes na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed.
Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.
Meneja wa Kadi wa benki hiyo, Philbert Casmir, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.
Meneja wa Kadi wa benki hiyo, Philbert Casmir, akitoa maelekezo jinsi ya kutumia mashine ya Pos maalumu yenye kuruhusu huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.
 ATM maalumu zenye kuruhusu huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.


Meneja wa Kadi wa benki hiyo, Philbert Casmir, akitoa maelekezo jinsi ya kutumia ATM maalumu zenye uwezo wa kuruhusu huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.
Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei, Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed, Mkurugenzi wa Huduma Rejareja na Biashara wa Barclays, Kumaran Parther kwenye picha ya pamoja.

Afisa wa Benki ya Barclays akitoa maelekezo jinsi ya kuitumia mashine ya Pos maalumu yenye kuruhusu huduma ya kadi ya China Union Pay ya Benki hiyo.

Mkuu wa Maendeleo ya Biashara wa Kadi ya Union Pay, Herman Botes, akiteta jambo na Mwakilishi wa Ubalozi wa China, Gao Wei, na Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages