Fate of the Furious yavunja rekodi ya dunia - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Thursday, April 20, 2017

Fate of the Furious yavunja rekodi ya dunia

Vin Diesel amesema hakutarajia mauzo ya aina hiyo

Filamu ya Fate of the Furious imevunja rekodi ya dunia ya kuwa filamu iliyouzwa sana baada ya kuzinduliwa rasmi.

Filamu hiyo, ambayo ni ya nane katika mwendelezo wa filamu za Fast & Furious, ilipata mauzo ya jumla ya $532.5m (£424.7m) duniani wikendi ya Pasaka.

Hayo ndiyo mauzo ya juu zaidi duniani kwa filamu yoyote siku zake za kwanza baada ya kuzinduliwa rasmi.

Filamu hiyo imepita mauzo ya $529m (£421.8m) rekodi ya awali iliyowekwa na Star Wars: The Force Awakens.

Mauzo hayo ya filamu hiyo nchini Marekani hata hivyo yalikuwa chini ukilinganisha na mauzo ya filamu iliyotangulia.

Furious 7 ilipata mauzo ya $147.2m (£117.3m) nchini Marekani ilipozinduliwa 2015.


Lakini filamu ya sasa imezoa $100.2m (£80m) pekee.

Dwayne Johnson ameigiza katika filamu hiyo ya Fate of the Furious

Licha ya kushuka kwa mauzo yake Marekani, filamu hiyo bado ilichangia sehemu kubwa ya mauzo ya filamu Marekani, ambapo ilichangia karibu theluthi mbili.

Mshindani wake wa karibu alikuwa The Boss Baby, ambayo iliuza $15.5m na kuwa ya pili.

Filamu za Fast & Furious zilianza kuuzwa 200.

Ufanisi wa filamu hii ya sasa ulichangiwa sana na China ambapo mauzo yake yalikuwa $190m (£151m) kwa siku hizo tatu.

Vin Diesel, ambaye ameigiza katika kila filamu ya Fast & Furious amesema anashukuru sana na amefurahishwa sana na ufanisi wa filamu hiyo.

Wengine walioigiza katika Fate of the Furious ni Charlize Theron, Tyrese Gibson na Ludacris.

Filamu nyingine za Furious zitatolewa mwaka 2019 na 2021.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages