MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MAJENGO YA HOSTEL ZA WANAFUNZI UDSM - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Friday, April 14, 2017

MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MAJENGO YA HOSTEL ZA WANAFUNZI UDSM


Mradi wa Ujenzi wa Mabweni unaosimamiwa na Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA), uliopo Chuo Kikuu cha Dar es salaam unatarajiwa kukamilka hivi karibuni.

Hayo yamesemwa mapema hii leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda mara baada ya kufanya ziara ya ukaguzi katika mradi huo.

Amesema kuwa kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa mabweni hayo kutapunguza gharama kubwa ambayo wamekuwa wakiipata wanafunzi wa chuo hicho kupanga vyumba mitaani.

Aidha, Makonda ameongeza kuwa anajisikia fahari kubwa kufanya kazi chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwa anatimiza ahadi zake za kukamilisha Miradi mbalimbali katika Jiji la Dar es salaam ukiwemo mradi wa ujenzi wa mabweni hayo ya wanafunzi katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam.

Mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 yaliyounganishwa kimuundo wa ghorofa nne, yanatarajiwa kusaidia kupunguza gharama za malazi kwa wanafunzi wengi wa chuoni hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akisalimiana na Afisa Mahusiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jackson Isdory alipotembelea na kukagua majengo ya hostel za wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), yanayojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mapema leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akipatiwa maelezo na mmoja wa wakandarasi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akitaka kujua jambo kutoka kwa Afisa Mahusiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jackson Isdory kuhusu maendeleo ya ujenzi wa majengo hayo alipotembelea na kukagua majengo ya hostel za wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), yanayojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mapema leo.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akikagua baadhi ya Vitanda vilivyopo katika Hosteli hizo, mapema leo. 

Afisa Mahusiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jackson Isdory akifafanua jambo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa majengo hayo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda alipokwenda kutembela na kukagua majengo hayo.


Baadhi ya majengo ya hosteli za wanafunzi wa UDSM zinazojengwa.
Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akijadili jambo na baadhi ya wawakilishi na viongozi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akiongea na waandishi wa habari alipotembelea na kukagua majengo ya hostel za wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), yanayojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mapema leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akikagua baadhi ya Bafu na Vyoo vilivyopo katika Hosteli hizo, mapema leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akitoa maelekezo kwa afisa Mahusiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jackson Isdory. 

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages