Tuesday, April 25, 2017

Tamasha la muziki la MTN BUSHFIRE 2017 rasmi kufanyika Mei 26-28 Nchini Swaziland
Tayari tamasha
kubwa la Muziki linalofanyika kila mwaka mwezi Mei, nchini Swazland
linalojulikana kama MTN Bushfire limezinduliwa rasmi wiki iliyopita huku
kwa sasa likisubiriwa kwa hamu kufanyika hiyo Mei 26-28. 2017,nchini humo.
Tamasha hilo ambalo
kila mwaka linakuwa ni la kuvutia na lenye mvuto wa aina yake, ni miongoni
mwa matamasha makubwa Barani Afrika ambalo upaswi kurikosa kabisana tayari
tiketi za za tamasha hilo zimeanza kuuzwa kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa
mtandao (Online)
Kwa mwaka huu mbali
na jukwaa kuu, pia kutakuwa na jukwaa maalum la “MTN Bushfire Firefly STAGE”,
kwa udhamini wa MTN, ambapo itakuwa ni maalum kutoa nafasi kwa wasanii
chipukizi na wa ndani ya Swaziland ambao watapata kuonesha vipaji vyao.
“Jukwaa hili
litajumusha wasanii wa vikundi zaidi ya 100 ambao ni wa ndani pekee na
wataonesha ushindani wao na Mei 5,2017, vikundi vitatu ambavyo
vimefanya vizuri vitachaguliwa kushiriki MTN Bushfire 2017” ilieleza taarifa
hiyo.
Kwa wasanii wapya
watakaopamba jukwaa hilo kwa mwaka huu ambao tayari wametangazwa ni pamoja na:
Zahara, Mozambiques The Mute Band, Aero Manyelo, Spoek Mathambo’s Batuk
Collective, American acapella group.
Wengine ni Hugh
Masekela, Tkzee, Jah Prayzah, GoodLuck, Jermemy Loops, Faada Freddy, The
Kiffness, Matthew Mole, Baloji, Bombino, Jojo Abbot na wengine wengi.
Kwa upande wa Madjs
ni pamoja na DJ Fred Spider (France), Karla Kenya (Swaziland/Germany/USA),
Itallo Dlamini (Swaziland), Vukazithathe (South Africa), Easy Freak
(South Africa) Bholoja (Swaziland) , Hanwah (UK), Dusty & Stones
(Swaziland), Lodanda (Swaziland), Nicholas Ellenbogen’s Theatre for Africa
(South Africa).
Tags
# BURUDANI
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRIL 25, 2016
Older Article
WAUGUZI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI WASHEREHEKEA GET TOGETHER PARTY 2017
RAIS MWINYI: ASANTENI WASANII WOTE KWA KUNIUNGA MKONO
Hassani MakeroJan 24, 2025Light Upon Light Summit in Zanzibar Set to Inspire and Unite Global Muslim Community12th & 13th October 2024.
kilole mzeeSept 30, 2024BENDI ZA MUZIKI WA DANSI KUWASHA MOTO TAMASHA LA USIKU WA WAFIA DANSI JIJINI DAR ES SALAAM
Hassani MakeroMay 12, 2022
Labels:
BURUDANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment