Benki ya
Exim Tanzania hivi karibuni imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa wanafunzi
waliokuwa wanafanya ziara ya kimasomo kutoka chuo kikuu maarufu cha biashara
cha Marekani – Harvard Business School. Wanafunzi hao walikuja katika benki
hiyo jijini Dar es Salaam kwa wiki moja kama sehemu ya mafunzo yao ya mwaka wa
kwanza kupitia mpango unaoitwa ‘FIELD Global Immersion’ ambayo Exim ni mmoja wa
wanachama.
“Tunajivunia
kufanya kazi pamoja na chuo cha Biashara cha Harvard kwa kuwapatia wanafunzi
uzoefu wa kihalisia wa kufanya kazi katika nchi kama Tanzania”
alisema Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Fredrick Kanga. “Tuna uhakika kupitia ziara hii
wanafunzi hawa waliweza kupata ujuzi ambao wasingeweza kupata katika
majadiliano ya darasani pekee.”
Mpango
huo wa FIELD Global Immersion ni programu iliyoundwa kuwaimarisha wanafunzi na
kuwajengea uwezo wao wa kumudu na kuweza kufanya kazi kiufanisi katika tamaduni
mbalimbali ulimwenguni.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu
maarufu cha biashara cha Marekani – Harvard wakizungumza na wananchi.
Benki ya
Exim ilianza kufanya kazi na wanafunzi hao kwa miezi kadhaa kabla ya kuwasili
nchini. Wakiwa nchini wanafunzi hao walitoa mawazo yao kwa uongozi, walishiriki
katika utafiti na wateja jijini Dar es Salaam na mwishowe kutoa mapendekezo yao
kwa uongozi wa benki. Kusudio la zoezi hili ni kutoa fursa kwa wanafunzi kupata
uzoefu wa kufanya kazi katika mradi wa uvumbuzi katika mazingira mageni.
Harvard
inakiri pia kuwa ziara hii ya kimasomo isingewezekana bila kuwepo na washirika
wa kimataifa. “Tunaishukuru
sana Exim Bank Tanzania na washirika wengine wote wa FIELD Global Partner kwa
yale wanayofanya kwa niaba ya wanafunzi wetu,” alisema Profesa Juan Alcacer, mkuu wa kitengo cha FIELD. “Wanafunzi
wetu wanafaidika kupita kiasi kupitia ziara hizi na tunategemea kuwa washirika
wetu wanafaidika pia.”


No comments:
Post a Comment