Tuesday, May 2, 2017

UPELELEZI KESI YA WEMA SEPETU WAKAMILIKA
Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa kesi ya kukutwa na bhangi inayomkabili
Msanii maarufu nchini wa filamu, Wema Isaack Sepetu (28) na wenzake wawili
umekamilika.
Wakili wa
Serikali, Onolina Moshi aliyaeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas
Simba wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.
Mheshimiwa,
kesi hii leo imekuja kwa ajili ya kutajwa lakini upelelezi umekamilika naomba
ahirisho kwa ajili ya kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali (PH). Amesema
Moshi.Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Juni Mosi, 2017 kwa PH.
Wema
amewakilishwa mahakamani hapo na Wakili Tundu Lissu.
Mbali na Wema
washtakiwa wengine ni mfanyakazi wake wa ndani, Angelina Msigwa (21) na Matrida
Seleman Abbas (16) aliyetambuliwa kuwa ni mkulima.Watuhumiwa hao wawili
wanatetewa na wakili Peter Kibatala na Hekima Mwesigwa.
Wema ambaye
ni mshindi wa taji ya Urembo wa Tanzania (Miss Tanzania) mwaka 2006 alifikishwa
mahakamani hapo na kupandishwa kizimbani baada ya kusota mahabusu katika kituo
kikuu cha Polisi (Police Central) Dar es Salaam kwa muda wa siku Sita.
Awali
ilidaiwa kuwa, Februari 4 mwaka huu, huko Kunduchi Ununio, wilaya ya Kinondoni,
washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja wa bangi na vipande viwili.
Hata hivyo
washtakiwa hao wote walikana mashtaka hayo na wapo nje kwa dhamana.
Tags
# FILAMU
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
RAIS WA ZANZIBAR AMEKUTANA NA MUIGIZAJI WA FILAMU ZA KIHINDI
Hassani MakeroNov 09, 2021Serikali Kuanzisha Mfuko Wa Sanaa Na Utamaduni-Dkt.Abbasi
Hassani MakeroJul 09, 2020MATOKEO YA TUNZO YA TANO YA FILAMU INAYOTOLEWA NA MFUKO WA EMERSON'S ZANZIBAR FOUNDATION KUTANGAZWA JULAI 4
Hassani MakeroJul 02, 2020
Labels:
FILAMU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment