Mwanamuziki Mose Fan Fan aliyeimba wimbo 'papa lolo' amefariki akiwa na miaka 75 - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Saturday, May 4, 2019

Mwanamuziki Mose Fan Fan aliyeimba wimbo 'papa lolo' amefariki akiwa na miaka 75


Mwanamuziki maarufu nchini DR Congo Mose Fan Fan amefariki akiwa na umri wa miaka 75.

Mwanamuziki huyo alifariki kutokana na kile kinachodaiwa huenda ni shtuko wa moyo nyumbani kwake karibu na barabara kuu ya Thika jijini Nairobi.

Mtunzi huyo wa wimbo 'Papa Lolo' uliotia fora alikuwa mjini Nairobi katika mradi wa kurekodi nyimbo mpya na wanamuziki wa Nairobi akiwemo Paddy Makani na Disco Longwa.

''Mose alikuwa akicheza Gita na bendi ya Franco Ok Jazz mwaka 1972. Ninamtambua kuwa mchezaji Gita na mwandishi mzuri wa nyimbo barani Afrika . Amekuwa akizuru Nairobi mara kwa mara tangu 2015 akishirikiana na na bendi ya Ketebul Music na tabu Osusa'' , alisema mshindi wa tuzo ya kuchora wanasesere paul Kelemba aka Mado kulingana na gazeti la The standard nchini Kenya.

Na mashabiki wa mwanamuziki huyo waliomboleza kifo chake muda tu habari zake zilipoanza kusambaa katika vyombo vya habari.




Mose alipenda sana Nairobi na amekuwa akitembea Kenya kila mwaka katika kipindi cha miaka mitatu iliopita kutoka London anakoishi.

''Tumeshangazwa na kifo chake na tunafanya mipango ya kumpeleka katika chumba kizuri cha kuhifadhi maiti huku tukiwasiliana na familia yake'', alisema Osusa.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages