Banda la Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania TWCC likiwa katika muonekao wa kuvutia na kupenda kwa watu mbalimbali wanaofika kwenye maonyesho ya Biashara ya 44 maarufu Sabasaba.
Watu mbalimbali wakiingia na kutoka ndani ya Banda la Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania TWCC kwenye maonyesho ya Biashara ya 44 maarufu Sabasaba.
Kaimu Mkurugenzi Mtengaji wa TWCC Mwajuma Hamza mwenye nguo ya ‘draft’ wapili kushoto akijadiliana jambo na baadhi wa wanachama wa chama hicho kwenye maonyesho ya biashara ya 44 ya Sabasaba, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Roses Wine Adelina Mwampamba.
Mjasiliamali na Kaimu Mkurugenzi wa Roses Wine Adelina Mwampamba akifurahia muonekano wa majani ya Rosela kwenye maonyesho ya Sabasaba Dar es Salaam, kulia kwake ni Mkurugenzi wa TWCC Mwajuma Hamza na wanachama wengine wa chama hicho.
Mjasilimali wa Korosho Tatu Matango mwenye nguo nyeusi akitoa maelezo namna ya uandaaji na ufungashaji wa bidhaa hiyo kwa watu mbalimbali waliotembelea Banda la TWCC kwenye maonyesho ya biashara ya 44 ya Sabasaba.
Mjasilimali wa Korosho Tatu Matango mwenye nguo nyeusi akikabidhi bidhaa hiyo kwa mnunuzi aliefika kwenye Banda la TWCC kwenye maonyesho ya biashara ya 44 ya Sabasaba
No comments:
Post a Comment