WAFANYABIASHARA GOBA WAOMBWA KUTOA USHIRIKIANO KWA TRA - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Monday, May 19, 2025

WAFANYABIASHARA GOBA WAOMBWA KUTOA USHIRIKIANO KWA TRA

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Kikodi Tegeta Bw Dickson Qamara amewataka wafanyabiashara wa Goba kutoa ushirikiano kwa maafisa wa TRA wanaopita katika maeneo yao ya biashara kwa lengo la kutoa elimu ya kodi na kusikiliza changamoto zao kwa lengo la kuboresha huduma zao.

Bw. Qamara ameyasema hayo leo tarehe 19.05.2025 alipokutana na maafisa watakaoshiriki zoezi hilo la mlango kwa mlango ofisini kwake Tegeta, jijini Dar es Salaam.

Bw. Qamara amewashukuru walipakodi kwa kuendelea kulipa kodi vizuri akiahidi kuendelea kuboresha huduma zao ili kurahisisha ulipaji kodi wa hiari.
Nae Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi ambae ni kiongozi wa timu hiyo CPA Paul Walalaze amesema katika zoezi hilo wamejipanga kuwaelimisha wafanyabiashara juu ya mambo mbalimbali ya kodi kama vile usajili wa biashara, wajibu wao wa kutoa na kudai risiti za EFD, kufanya makadirio na kufanya malipo ya kodi ya awamu ya pili.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages