Balozi Asha Rose Migiro ampongeza Mwanariadha Alphonse Simbu - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, April 26, 2017

Balozi Asha Rose Migiro ampongeza Mwanariadha Alphonse Simbu

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro leo aliandaa hafla fupi katika makazi ya Balozi kumpongeza kijana mtanzania Alphonse Simbu Kwa kushika nafasi ya tano katika mbio za "London Marathon" zilizofanyika tarehe 23 Aprili 2017 jijijini London.

Katika salamu zake, Balozi Migiro alimpongeza Bw. Simbu kwa heshima aliyoipa Tanzania jijini London na Duniani  kupitia mbio za London. alimsihi atumie matokeo hayo kama hamasa ya  kufanya bidii zaidi kwa ajili ya mashindano ya mbio ndefu anayotarajiwa kushiriki baadae mwakani.


Simbu alimshukuru Balozi Migiro Kwa ushirikiano mkubwa wa kibalozi alioupata akiwa jijini London. Alimkabidhi Balozi Fulana ya kumbukumbu ya ushiriki wake kwenye mbio hizo.

Pichani Balozi Asha Rose Migiro akipokea Fulana hiyo.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages