MWANAFUNZI WA SHULE YA KIMATAIFA TANGANYIKA ALIVYOELEZEA SIASA KATIKA SANAA YA UCHORAJI - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Thursday, April 20, 2017

MWANAFUNZI WA SHULE YA KIMATAIFA TANGANYIKA ALIVYOELEZEA SIASA KATIKA SANAA YA UCHORAJI

Mwanafunzi Samwel Malebo (16) anayesoma shule ya kimataifa ya Tanganyika grade 10 alivyoelezea siasa ya Tanzania kwa sasa katika sanaa ya uchoraji kwa kutumia michoro mbalimbali ya inayoelezea siasa katika nyanja tatu za Demokrasia, Rushwa na Utawala Bora.

Katika michoro yake aliyoichora kwa ubunifu na kipaji cha hali ya juu kaielezea vizuri sana siasa katika kidemokrasia, rushwa na Utawala bora. Akitoa maelezo kwa wanafunzi na wadau mbalimbali waliotembelea maonyesho hayo yaliyofanyika tarehe 11/02/2017 Makumbusho ya Taifa amelezea kilchomvutia kuchora michoro hiyo kuwa ni siasa ya Tanzania kwa sasa.

Akiongea na mwandishi alisema Kilichonivutia hadi kuchora micho ya kisiasa ni nilipata msukumo toka nikiwa shule ya msingi kwani nilikuwa nasikia mambo mbalimbali ya siasa lakini sikuwahi kufundishwa mambo haya, kwa sasa nimekuwa naona hali halisi ndio maana nikavutiwa kuchora michoro na kuelezea siasa kwa ujumla.

Katika maonesho hayo Jumla ya michoro kumi imeonyeshwa na imetoa taswira ya kisiasa katika demokrasia, rushwa na Utawala bora.

Ni vizuri kuwaendeleza vijana na kuwapa ushirikiano pale wanapoonyesha wana kitu cha ziada na ubunifu mzuri alisema mmoja ya wadau ambao wametembelea maonyesho hayo na kuyakubali.


Pia nikiongea na mama mzazi Bi. Leah Lugimbana amesema aligundua kipaji cha mwanawe toka akiwa mdogo kwa kuwa alikuwa anapenda kucho chora hivyo aliona kuna haja ya kukiendeleza na ndio maana anampa ushirikiano mkubwa.

Wanafunzi na watu mbalimbali walioona wamemsifia na kuelewa michoro kwa urahisi inachoelezea akiwemo mtalii wa Kimataifa ambaye ni Rais wa
 Shirika la Forodha Duniani Bwana Kunio Mikuriya amesema Nimefurahishwa na maonyesho ya mapambano dhidi ya rushwa katika kulijenga Taifa kwa faida ya wananchi pia ameonyeshw akustaajabishwa kwa jinsi kijana mdogo alivyoweza kuelezea kwa kutumia sanaa ya uchoraji.

 Samwel Malebo akimpa Maelezo Rais wa Shirika la Forodha Dunia 
Bwana Kunio Mikuriya picha zake zinazoelezea mapambano dhidi ya rushwa.
Samwel Malebo akiwaelezea wanafunzi wa Shule ya Msingi Barabara ya Mwinyi
Picha zake alizochora 
 Samwel Malebo akijadilaina na wanafunzi mbalimbali Kuhusiana na michoro yao na kujibu maswali mbalimbali
Samwel Malebo akiwa na mama yake Bi Leah Lugimbana Katika ufunguzi wa Maonyesho yake ya picha.
Baadhi ya michoro kati ya 10 iliyopo kwenye onyesho hilo.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages