Tuesday, April 25, 2017

WATANZANIA WAASWA KUWA WAZALENDO NA KULINDA AMANI ILIYOPO
Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Ajira na Wenye ulemavu,
Jenista Mhagama amewaasa Watanzania kuwa wazalendo pamoja na kudumisha amani na
utulivu uliopo nchini.
Akizungumza,
leo mjini Dodoma wakati akifuatatilia maandalizi ya Maadhimisho ya miaka 53 ya
Muungano yatakayofanyika Aprili 26 mwaka huu katika Uwanja wa Jamhuri uliopo
mjini Dodoma.
“Tunapoadhimisha
miaka 53 ya Muungano ninawaomba watanzania kuwa wazalendo pamoja na kulinda
amani ya nchi” alisema Waziri Mhagama
Pia, Waziri
Mhagama aliwaomba watanzania hasa wakazi wa Dodoma kuhudhuria kwa wingi katika
Maadhimisho hayo yatakayofanyika jumatano wiki hii.
Kwa upande
wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alisema kuwa mkoa wake
umejipanga vizuri katika kufanikisha maadhimisho hayo, ambapo pia alivishukuru
vyombo vya habari kwa kuhamasisha wananchi juu ya maadhimisho hayo.
“Wananchi
wamehamasika kushiriki katika maadhimisho haya ya miaka 53 ya Muungano, ninawashukuru
kwa kazi kubwa mliyoifanya na tunaamini mtaendelea kuhamasisha wananchi
kushiriki katika maadhimisho hayo” alisema Rugimbana
Maandalizi ya
Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano yamehudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya ya
Dodoma mjini Christina Mndeme, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali.
Aidha, Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa
mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, ambapo pia yatahudhuriwa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohammed Shein na
viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.
Maadhimisho
hayo ya miaka 53 ya Muungano yanatarajiwa kupambwa namaonesho kutoka kutoka
vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama, burudani za vikundi vya ngoma pamoja
na maonesho ya halaiki.
Waziri Mhagama akikagua maandalizi ya kuadhimisha Sherehe za Miaka 53 ya
Muungano katika viwanja vya Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Baadhi ya wananchi
wakifuatilia maonesho ya maandalizi ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe 26 Aprili Mjini Dodoma
kwa mara ya kwanza tangu Serikali ilipohamia Dodoma.
Vikosi vya Ulinzi na
Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya maadhimisho ya Maadhimisho ya
miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe
26 Aprili Mjini Dodoma.
Vikosi vya Ulinzi na
Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya maadhimisho ya Maadhimisho ya
miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe
26 Aprili Mjini Dodoma.
Vikosi vya Ulinzi na
Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya maadhimisho ya Maadhimisho ya
miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe
26 Aprili Mjini Dodoma.
Askari wa Pikikipi
maalum wakionesha namna pikipiki hizo zitakavyopamba maonesho hayo.
Makomandoo wa Jeshi
la wananchi wa Tanzania wakionesha umahiri wao wa kuvuta gari lenye tani 7
ikiwa ni moja ya mbinu ya medani katika uwanja wa mapambano.
Askari wa Kikosi cha
Farasi wakionesha umahiri wao katika kutumia farasi kupambana na uhalifu.
Wanafunzi wa halaiki
wakipita kwa ukakamavu mbele ya Jukwaa Kuu.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
SHIRIKA LA ANGA LA ETIHAD LAMTEUA ROBIN KAMARK KUWA OFISA MTENDAJI MKUU WA IDARA YAKE TANZU YA AIRLINE EQUITY PARTNERS
Older Article
BENKI YA BARCLAYS TANZANIA LIMITED YAKUZA UCHUMI WA VIJANA KUPITIA MFUMO ENDELEVU WA HUDUMA ZA JAMII
SERIKALI YATOA MWEZI MMOJA KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE 2024 KUBADILISHA MACHAGUO YA TAHASUSI ZA KIDATO CHA TANO
Hassani MakeroApr 02, 2025WADAU WAOMBWA KUJITOKEZA KUDHAMINI TAMASHA LA KUOMBEA UCHAGUZI MKUU MWAKA HUU
Hassani MakeroApr 02, 2025Rais Samia ahutubia Baraza la Eid El Fitr Jijini Dar es Salaam
Hassani MakeroMar 31, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment