Serengeti Boys yaichapa Cameroon - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Monday, May 1, 2017

Serengeti Boys yaichapa Cameroon


Timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya miaka 17 'Serengeti Boys

TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imeendeleza wimbi la ushindi katika mechi zake za kujipima nguvu katika mechi za kimataifa katika maandalizi ya kujiandaa na mashindano ya AFCON kwa vijana chini ya miaka 17 yatakayoanza mwezi Mei 14, 2017 baada ya jana kuwafunga wenyeji, Cameroon 1-0 mjini Yaounde.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Ahmadou Ahijo, mjini Yaounde na kuhudhuriwa na gwiji wa soka wa Cameroon, Rogger Milla, bao la Serengeti Boys limefungwa na Ally Ng'anzi dakika ya 36.

Serengeti Boys ilitua Younde, Cameroon Alhamisi ikitokea mjini Rabat, Morocco ambako iliweka kambi ya karibu mwezi mmoja na kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Gabon na kushinda 2-1 kila mchezo.

Kwa ujumla Serengeti Boys imekwishacheza mechi tano tangu kuanza kambi rasmi ya maandalizi fainali za Gabon, baada ya awali kuifunga Burundi mara mbili, Machi 30 mabao 3-0 na Aprili 1 mabao 2-0, mechi zote mbili zikipigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, kabla ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Ghana ‘Black Starlets’ Aprili 3 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Baada ya mchezo wa leo, Serengeti Boys inatarajiwa kurudiana na Cameroon Mei 3, mwaka huu kabla ya Mei 7 kwenda Gabon ambako imepangwa kundi B pamoja na timu za Mali, Niger na Angola.


Cameroon nayo itashiriki fainali hizo ikiwa imepangwa Kundi A lina timu za wenyeji, Gabon, Guinea na Ghana.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages