Shein aipongeza Benki ya NBC - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Tuesday, June 5, 2018

Shein aipongeza Benki ya NBC

Rais wa Zanzibar  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein (wa pili kushoto), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Theobald Sabi katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake mjini Zanzibari hivi karibuni.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe.Ayoub Mohamed Mahmoud (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji NBC Bw.Theobald Sabi wakati alipofika Zanzibar Beach Resort jana katika Futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC hapa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akichukua chakula cha futari iliyoandaliwa na  Benki ya NBC hapa Zanzibar katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort (kulia) Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe,Zubeir Ali Maulid.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali wakichukua chakula cha futari iliyoandaliwa na  Benki ya NBC hapa Zanzibar katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar.
Baadhi ya Wateja wa Benki ya NBC hapa Zanzibar walioalikwa katika futari iliyoandaliwa jana katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, ambapo mgeni rasmi alikuwa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha na Uongozi wa Benki ya NBC mara baada ya Futari waliyoiandaa jana katika
Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, akiwepo na 
Mkurugenzi wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein (wa tano kushoto)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) alipokuwa akiagana na Viongozi wa Benki ya NBC mara baada ya Futari waliyoiandaa katika
Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, hafla iliyohudhuriwa na Viongozi mbali mbali na Wananchi.


Rais wa Zanzibar  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein ameipongeza Benki ya NBC kutokana na kasi yake na juhudi za kukuza uchumi wa Zanzibar.

Akizungumza kwa niaba ya rais wa Zanzibar katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo iliyofanyika mjini Zanzbar hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud amesema pato la taifa limekuwa likikuwa mwaka hadi mwaka kutokana na mchango unaotolewa na taasisi mbali mbali ikiwemo Benki ya NBC.

Aidha Dk.Shein ameihimiza benki hiyo kuendelea na juhudi zake za kuimarisha mazingira bora na huduma kwa wateja wake ili kwenda sambamba na kasi ya mabadiliko ya huduma za kifedha yanayotokea siku hadi siku na kukuza maendeleo bora nchini.

Hata hivyo ameipongeza Benki hiyo kwa kuonesha umuhimu kwa wateja wake kwa kurejesha miongoni mwa faida wanazozipata ikiwemo kwa njia hiyo ya kufutarisha na kutoa huduma nyengine mbali mbali kwa jamii.

Awali akizungumza katika hafla hiyo ya futari Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBC,  Dk. Kassim Hussein amesema kukuwa kwa huduma za kifedha Zanzibar pia kunatokana na huduma bora zinazotolewa na benki hiyo inayokwenda sambamba na mahitaji ya wateja wake.

Amesema mazingira salama yaliopo Zanzibar yanayoimarishwa na viongozi wakuu wa nchi imewezasha benki hiyo kufanya kazi zake za kutoa huduma za kifedha kwa ufanisi na umakini Zaidi.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages