MKE WA RAIS WA ZANZIBAR MAMA MWANAMWEMA SHEIN AJUMUIKA NA WATOTO WA KIJIJI CHA SOS KATIKA FUTARI ALIYOWAANDALIA - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, May 29, 2019

MKE WA RAIS WA ZANZIBAR MAMA MWANAMWEMA SHEIN AJUMUIKA NA WATOTO WA KIJIJI CHA SOS KATIKA FUTARI ALIYOWAANDALIA

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akijumuika na Watoto wa Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar, katika Futari Maalum aliyowaandalia katika makazi yao iliofanyika juzi 27-5-2019. 

WATOTO wa Kijiji cha Watoto SOS Mombasa Zanzibar wakipata futari walioandaliwa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na kujumuika nae katika hafla hiyo ya futari iliofanyika juzi 27-5-2019, katika makazi yao Mombasa Zanzibar.) 
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, kushoto Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi na kulia Waziri wa Kazi Uwezeshaji wa Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Mhe. Maudline Castico, wakijumuika na Watoto wa Kijiji cha Watoto cha SOS Mombasa Zanzibar, katika futari Maalum walioandaliwa na Mama Mwanamwem,Shein, katika makaazi yao.

WATOTO wa Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar wakijumuika na Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein, katika futari maalum aliyowaandalia katika makaazi yao.
MKURUGENZI wa Kijiji cha Watoto cha SOS Mombasa Zanzibar Bi. Asha Salum Ali, akitowa neno la shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya futari maalum ilioandaliwa katika makaazi yao.
MTOTO Mohammed Ali Dausi akisoma dua baada ya kumalizika kwa hafla ya Futari Maalum walioandaliwa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, iliofanyika katika makaazi ya SOS Mombasa Zanzibar 
MKE wa Rais wa Zanzibaerv Mama Mama Mwanamwema Shein, akiitikia dua ikisomwa na Mtoto wa Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar Mohammed Ali Deus, baada ya kumalizika kwa hafla ya futari iliofanyika katika ukumbi wa SOS Mombasa Zanzibar kushoto Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi na kulia Waziri wa Kazi, Uwezeshaji wa Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe Maudline Castico.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akimsalimiana mmoja wa Watoto Wanaolelewa katika Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar Wahida Abdallah, aliyebebwa na mtoto mwezake Amina Shabani, baada ya kumalizika kwa kwa hafla ya futari aliyowaandalia katika makaazi yao SOS Mombasa Zanzibar.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na kuagana na Watoto wa Kijiji cha SOS Mombasa Zanzibar, baada ya kumaliza hafla ya futari aliyowaandalia katika makaazi yao Mombasa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages