Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, amewataka watumiaji wa barabara ya Morogoro kutumia njia ya barabara ya msata baada ya kutokea ajali ya magari manne katika daraja la Mkalamo Mlandizi.
Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Julai 02,2020 imesababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi watatu.
Tukio hilo limesababisha kuwepo kwa foleni kubwa na polisi kuifunga barabara hiyo kwa muda kutokana na ajali hiyo.
Kamanda Nyigesa amesema Jeshi la polisi mkoani Pwani linaendelea na jitihada za kutoa magari hayo yaliyofunga njia.
Habari za awali inadaiwa kuwa lori la mafuta limegongana na gari jingine na kusababisha magari mawili kugongana katika eneo hilo.
Habari hii itaendelea..
No comments:
Post a Comment