Thursday, July 9, 2020

REA YAWASHA UMEME KWENYE VIJIJI ZAIDI YA 9000 NCHINI
Ofisa Uhusiano wa Wakala wa Nishati Vijijini REA Jaina Msuya (wa katikati) akitoa Elimu kwa mgeni aliyefika kwenye banda lao kwaajili ya kufahamu shughuli mbalimbali zinazofanywa na REA, kushoto kwake ni Mtaalam wa upimaji wa nguzo Saum Mohamed kutoka katika Kiwanda cha kutengeneza nguzo cha Qwihaya general enterprises company ltd kilichopo Mafinga Iringa, na kulia kwake ni Benedict Marealle kutoka ktoka kwenye kapuni ya Baobab Energy System.
Ofisa Uhusiano wa Wakala wa Nishati Vijijini REA Jaina Msuya (wa katikati) akitoa Elimu kwa mgeni aliyefika kwenye banda lao kwaajili ya kufahamu shughuli mbalimbali zinazofanywa na REA, kushoto kwake ni Mtaalam wa upimaji wa nguzo Saum Mohamed kutoka katika Kiwanda cha kutengeneza nguzo cha Qwihaya general enterprises company ltd kilichopo Mafinga Iringa.
Mwelimishaji wa Teknolojia ya Sumaku akitoa maelezo kwa watu waliofika kwenye banda la REA katika Maonyesho ya 44 ya Biashara Maarufu kama Sabasaba kujionea Teknolojia hiyo inavyoweza kuwasha jiko la kupikia.
Ofisa kutoka kampuni ya ENVOTEC inayojishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa Majiko ya Gesi Salama Sudi akitoa elimu kuhusu ufanisi wa bidhaa ya kwa mwananchi aliefika kwenye banda la REA kujionea shughuli mbalimbali zilizopo kwenye banda hilo katika Maonyesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba.
Bi Regina David Ofisa kutoka kwenye Kampuni inayojihusisha na usambazaji wa Mita maalum zenye uwezo wa kupima ujazo wa Gesi ya KOPA GAS (kushoto), akitoa maelezo kuhusu Mita hizo namna zinavyofanya kazi kwa watu aliefika kwenye banda la REA kujionea shughuli mbalimbali zilizopo kwenye banda hilo katika Maonyesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasab.
Dar es Salaam: Wakala wa Nishati Vijijini REA imesema kuwa hadi kufikia mwezi Juni mwaka 2021 Vijiji vyote vilivyosalia kufikishiwa Umeme vinatakiwa kukamilika kwa kufikiwa na Nishati hiyo.
Ofisa habari wa REA Jaina Msuya amebainishaa hilo kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika kwenye Maonyesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba ambapo amesema kuwa mpaka sasa Zaidi ya vijiji 9000 nchi nzima tayari vimefikiwa na Umeme.
Aidha ameongeza kuwa wakati REA inaanzishwa Mwaka 2007 kulikua na Vijiji 502 tu vilivyokuwa na umeme kati ya vijiji 12,268 nchi nzima, ambapo mpaka sasa zaidi ya Vijiji 300 ndivyo vilivyosalia kupatiwa nishati hiyo na kwamba wanakaribia kutangaza Zabuni kwa wakandarasi ili kuweza kukamilisha kazi hiyo.
“Kuna jumla ya Vijiji 12,268 nchini na tayari zaidi ya Vijiji 9000 vimefikiwa na Umeme sasa imebaki kazi ya kutangaza zabuni kwa wakandarasi ili kuweza kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Juni 2021” alisema Ofisa habari huyo Jaina.
Aidha ametoa mwito kwa watu mbalimbali wanaoishi kwenye Vijiji vilivyopatiwa Umeme kuchangamkia fursa hiyo kwa kuanzisha shughuli za uzalishaji mali kwa kuanzisha Viwanda vidogovidogo ili kujiongezea kipato.
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
RC MAKONDA AMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA MAPINDUZI MAKUBWA YA UJENZI WA RELI YA KISASA YA SGR.
Older Article
TASAC YATARAJIA KUTOA GAWIO KWA SERIKALI ZAIDI YA SH. BILIONI 20
Absa Group Reports 10% Increase in 2024 Earnings after Material Second-Half Recovery
Hassani MakeroMar 11, 2025Benki ya NBC Yaandaa Hafla ya Futari Zanzibar, Yajivunia Ongezeko la Wateja
Hassani MakeroMar 07, 2025BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA RASHAL ENERGIES, INAYOJENGA BOMBA LA GESI KISEMVULE-MBAGALA
Hassani MakeroMar 07, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment