Friday, July 10, 2020

Home
KITAIFA
RC MAKONDA AMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA MAPINDUZI MAKUBWA YA UJENZI WA RELI YA KISASA YA SGR.
RC MAKONDA AMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA MAPINDUZI MAKUBWA YA UJENZI WA RELI YA KISASA YA SGR.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amefanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Reli Mpya ya Kisasa ya Standard gauge kwaajili ya Usafiri wa Treni Umeme inayoanzia Dar es salaam hadi Makutupora Dodoma na kumpongeza Rais Dkt. John Magufuli kwa mapinduzi makubwa kwenye usafiri wa Reli.
Akiwa kwenye Ujenzi wa Jengo la Abiria ambalo ujenzi wake umefikia 80%, RC Makonda amewataka Wafanyabiashara kuanza kuchangamkia fursa ya kufungua Biashara mbalimbali kwenye Jengo hilo la Gorofa nne ikiwemo Supermarket, Maduka, Migahawa, Mall's na huduma za kifedha ikiwemo Bank na Mitandao ya Simu.
Aidha RC Makonda amesema kwa sasa Serikali ipo kwenye hatua ya kuanza ujenzi wa Reli kwaajili ya Treni ya katikati ya mji ikianzia Kerege Bagamoyo hadi maeneo ya mjini ikiwemo posta kwa lengo la kurahisisha shughuli za usafiri.
Kwa Mujibu wa Shirika la Reli Tanzania TRC ujenzi wa Reli kutoka Dar es salaam, Morogoro hadi Dodoma Makutupora unagharimu zaidi ya Shilingi Trillion 7.2.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
BALOZI WA UJERUMANI NCHINI ATEMBELEA BANDA LA TUME YA MADINI KWENYE MAONESHO YA SABASABA
Older Article
REA YAWASHA UMEME KWENYE VIJIJI ZAIDI YA 9000 NCHINI
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment