RAIS DK.MWINYI AJUMUIKA NA WANANCHI KATIKA MAZIKO YA ALIYEWAHI KUWA MKURUGENZI WA ZIPA ZANZIBAR - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Saturday, January 22, 2022

RAIS DK.MWINYI AJUMUIKA NA WANANCHI KATIKA MAZIKO YA ALIYEWAHI KUWA MKURUGENZI WA ZIPA ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Kiislam katika Sala ya kusalia Jeneza la marehemu Salum Khamis Nassor, iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Zanzibar na (kushoto kwa Rais) Rais Mstafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Mstafu Alhaj Balozi Seif Ali Iddi wakijianda kubeba jeneza kwa ajili ya Ibada ya kusalia Mwili wa Marehemu.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ya kumuombea Marehemu Salum Khamis Nassor, ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi, baada ya kumalizika kwa Sala ya Jeneza, iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Zanzibar na (kushoto kwa Rais) Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Mstaafu Alhaj Balozi Seif Ali Iddi na (kulia kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, wakiitikia dua.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kumpa mkono wa pole Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Ibada ya kusalia jeneza la Marehemu Salum Khamis Nassor, aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji ZIPA, Ibada hiyo iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Zanzibar leo 22-1-2022. (Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages