WATU 13 WATAKIWA KUFIKA KITUO CHA KATI WAKIWA NA MITAMBO YAO YA KUZALISHA KAZI ZA WASANII - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Thursday, April 20, 2017

WATU 13 WATAKIWA KUFIKA KITUO CHA KATI WAKIWA NA MITAMBO YAO YA KUZALISHA KAZI ZA WASANII

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataja watu 13 wenye mitambo ya kufyatua kazi za wasanii wa nje na ndani ya nchi yetu  wakutane kituo cha polisi cha kati wakiwa na nyaraka halali za kufanyia kazi hiyo.

Akizungumza na wasanii hao pamoja na wananchi leo katika mkutano wa kupambana na maharamia wa kazi za wasanii,Makonda alisema kuna baadhi ya watu wanafanya kazi za bla bla kwa kuwanyonya wasanii.

Amesema kuanzia leo ni mwisho kwa wale wanaouza nyimbo za wasanii amesema wanaotakiwa kufanya hivyo niwale wenye mikataba halali na wasanii wenye nyimbo husika.

Makonda amesema kuwa kazi zote za wasanii na zinatakiwa ziwe na stika za Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ilinchi iweze kupata mapato na kukuza tasnia ya sanaa nchini.

Amesema kwa wale wanaouza kazi za wasanii mikononi zinatakiwa kuwa na stika za TRA Pamoja na kuwa na kibali maalum kutoka bodi ya filamu.

Hata hivyo amesema Makonda kunawatu wanafanya kazi za kuwarubuni wasanii na na kufanya maisha yao yawe duni katika hiyo wakati Nigeria inaongoza kwa kupata pesa nyingi kupitia filamu.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akizungumza na Wasanii waliofika Kariakoo mara baada ya maandamano ya kupinga Biashara ya uuzaji filamu za nje.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda katikati akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi. Bi. Joyce Fissoo wakati akizungumza katika mkutano huo.
 Baadhi ya wasanii waliohudhuria maandamano hayo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda na baadhi ya wasanii wa filamu, wasanii wa muziki pamoja na wasambazaji wa kazi za sanaa wakiongoza maandamano ya kupinga uingizwaji wa filamu za kigeni nchini bila kufuata taratibu
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda na baadhi ya wasanii wa filamu, wasanii wa muziki pamoja na wasambazaji wa kazi za sanaa wakiongoza maandamano ya kupinga uingizwaji wa filamu za kigeni nchini bila kufuata taratibu
 Kundi la Wasanii wakishangilia jambo kutoka kwa mkuu wa Dar es Salaam Paul Makonda
 Baadhi ya wasanii waliohudhuria kwenye maandamano hayo wakishangilia jambo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda akisalimiana na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la K.K.K.T Usharika wa Kariakoo.
 Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Filamu nchini, Jimy Mafufu akizungumza kwa niaba ya wasanii katika mkutano huo.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa nchini (BASATA), Godfrey Mwingereza akizungumza na wasanii wa filamu waliofika katika maandamano hayo yaliyoitimishwa katika mtaa wa Mafia Kariakoo.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na Wasanii hao.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na wasanii katika mtaa wa Mafya mara baada ya kumaliza maandamano ya wasanii kupinga uuzwaji wa filamu za nje ambazo zinachangia kushuka kwa thamani ya filamu za ndani kutokana na bidhaa hizo kutolipiwa kodi.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages