ATHARI ZA MVUA ZA MASIKA JIJINI DAR ES SALAAM - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Thursday, May 4, 2017

ATHARI ZA MVUA ZA MASIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Wakazi wa Kinondoni Mahakamani wamelalakia maji yaliyozingira nyumba zao kutokana na baadhi ya wakazi hao kujenga katika mkondo wa maji.

Akizungumza leo mkazi wa eneo Bi. Khadija Hamis amesema kutokana na mvua za masika zinazoendelea kunyesha wanapata adha ya maji hayo yanayotuama kwenye eneo hilo.

Amesema kuwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamezingirwa na maji kwa wiki mbili na hakuna chochote kinachofanyika.

Aidha amesema kutokana na hali hii kuendelea wanaiomba serikali kutatua tatizo hili mara baada ya kuisha masika.


Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam iliyoanza kunyesha wiki iliyopita, zimesababisha maafa, uharibifu wa miundombinu ya baarabara pamoja na baadhi nyumba katika eneo la Kinondoni Mahakamani kuzungukwa na maji ya mvua jijini Dar es Salaam.


Mwanafunzi akikwepa dimbwi la maji machafu ya mvua kama yanavyoonekana pichani leo jijini Dar es Salaam.




Wakati huo huo, mvua hizi zinazoendelea zimeendelea kuleta maafa na athari kubwa maeneo ya Ubungo Kisiwani nyuma ya hoteli maarufu ya Land Mark. Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamekosa makazi kwa kubomokewa na nyumba zao na kuomba serikali iwasaidie kutokana na hali iliyowakuta.

Akiongea na Wor’Out Media Blog, Mjumbe wa Mtaa wa Hekima Kata ya Ubungo Kisiwani Bondeni, Bi Tabu Selemani, anashangazwa na hali ilivyojitokeza kwa mvua hizi, kwani mara nyingi mafuriko huwa yanawatesa watu wa mabondeni tofauti na mvua hizi.


Mvua hizi zimeathiri sana nyumba zilizokuwa hazihisiwi kupata athari za mvua kwamiaka yote.”

 Maji yatamalaki kwenye viunga vya Mtaa wa Hekima, Ubungo Darajani
 Maji yatamalaki kwenye viunga vya Mtaa wa Hekima, Ubungo Darajani
 Maji yatamalaki kwenye viunga vya Mtaa wa Hekima, Ubungo Darajani
 Maji yatamalaki kwenye viunga vya Mtaa wa Hekima, Ubungo Darajani
 Wakazi wakitazama maji ya mto yalitapikwa na mto na kuzagaa kwenye makazi ya mtaa wa Hekima, kwa mjumbe Tabu Selemani.

 Maji yatamalaki kwenye viunga vya Mtaa wa Hekima, Ubungo Darajani nyumbani kwa Mjumbe wa Mtaa huo.















Tazama tofali za nyumba zilizo athiriwa na mafuriko hayo
Moja ya nyumba zilizoathiriwa na mvua hizi zinazoendelea jijini Dar es Salaam na kupelekea wakazi wake kukosa mahali pa kukaa
Mitaa yote imeathiriwa na kujaa matope baada ya maji yaliyojaa kwenye viunga vya makazi ya waishio bondeni kupungua

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages