INAHUZUNISHA ALIYEWAHI KUWA MKUU WA WILAYA SABA ATAPELIWA NYUMBA. - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Friday, February 2, 2018

demo-image

INAHUZUNISHA ALIYEWAHI KUWA MKUU WA WILAYA SABA ATAPELIWA NYUMBA.

IMG_5312
Mzee Waziri akionesha hati halali ya umiliki wa nyumba hiyo
IMG_5304
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya Saba hapa nchini adhulumiwa nyumba na mpangaji wake,baada ya kuuziwa na Mtu aliyetapeli nyumba hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Leo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya huyo mstaafu Waziri Juma amesema nyumba hiyo alikuwa akimpangisha mpangaji huyo ambaye Ni mchina,na alaikuwa akilipa kodi Kama ipasavyo lakini baada ya Muda akadai kuwa ameuziwa nyumba hiyo.

"Hii nyumba Ni kiinua mgongo changu na niliamua kuipangisha ili niweze kupata hela ya kunisaidia kimaisha katika wakati huu niliostaafu lakini nimedhulumiwa na mchina akidai ameinunua "amesema Juma Waziri. 

Aidha amebainisha kuwa kabla ya mpangaji huyo kuinunua nyumba hiyo ilikopwa fedha benki na Mtu asiyefahamika na walipofahamu walitoa taarifa kwa benki hiyo wasitoe mkopo huo lakini baadae ikaja onekana ilikopwa hela kwa nyumba hiyo kitu ambacho kiliwashangaza Sana 

Anaendelea kusema kuwa baada ya fedha hiyo kukopwa na Mtu asiyefahamika na ambaye Hakuna mwanafamilia alishindwa kurejesha mkopo huo,na kupelekea nyumba hiyo kuuzwa ili kulipa deni hilo la benki ndipo mpangaji huyo ambaye ni mchina aliinunua. 

"Mimi binafsi sijawahi kukopa benki wala kuuza nyumba maana hii nyumba inanisaidia kujikimu kipindi hiki cha uzeeni hivyo Naomba hawa walipfanya kitendo hiki waweze kuchukuliwa hatua."Amesema Juma. 

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages

Contact Form

Name

Email *

Message *