Friday, February 2, 2018

INAHUZUNISHA ALIYEWAHI KUWA MKUU WA WILAYA SABA ATAPELIWA NYUMBA.
Mzee Waziri akionesha hati halali ya umiliki wa nyumba hiyo
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya Saba hapa nchini adhulumiwa nyumba na mpangaji wake,baada ya kuuziwa na Mtu aliyetapeli nyumba hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya huyo mstaafu Waziri Juma amesema nyumba hiyo alikuwa akimpangisha mpangaji huyo ambaye Ni mchina,na alaikuwa akilipa kodi Kama ipasavyo lakini baada ya Muda akadai kuwa ameuziwa nyumba hiyo.
"Hii nyumba Ni kiinua mgongo changu na niliamua kuipangisha ili niweze kupata hela ya kunisaidia kimaisha katika wakati huu niliostaafu lakini nimedhulumiwa na mchina akidai ameinunua "amesema Juma Waziri.
Aidha amebainisha kuwa kabla ya mpangaji huyo kuinunua nyumba hiyo ilikopwa fedha benki na Mtu asiyefahamika na walipofahamu walitoa taarifa kwa benki hiyo wasitoe mkopo huo lakini baadae ikaja onekana ilikopwa hela kwa nyumba hiyo kitu ambacho kiliwashangaza Sana
Anaendelea kusema kuwa baada ya fedha hiyo kukopwa na Mtu asiyefahamika na ambaye Hakuna mwanafamilia alishindwa kurejesha mkopo huo,na kupelekea nyumba hiyo kuuzwa ili kulipa deni hilo la benki ndipo mpangaji huyo ambaye ni mchina aliinunua.
"Mimi binafsi sijawahi kukopa benki wala kuuza nyumba maana hii nyumba inanisaidia kujikimu kipindi hiki cha uzeeni hivyo Naomba hawa walipfanya kitendo hiki waweze kuchukuliwa hatua."Amesema Juma.
Tags
# KITAIFA
Share This
About kilole mzee
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Jero yako na Zantel yazidi kubamba
Older Article
WANANCHI WAMPONGEZA RC MAKONDA KWAKUONGEZA MUDA
Ni miaka minne ya neema kwa Mashirika ya Umma
Hassani MakeroMar 21, 2025INEC YATOA UFAFANUZI WANAOJIANDIKISHA ZAIDI YA MARA MOJA DAR
Hassani MakeroMar 20, 2025RAIS DKT. SAMIA ACHANGIA SH. MILIONI 50 KUMUENZI PADRI SHIRIMA
Hassani MakeroMar 20, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment