Monday, March 24, 2025

KAMPENI YA 'NO REFORM NO ELECTION' YAPOTEZA MWELEKEO RUKWA
Mkutano wa kampeni ya No Reform No Election unaoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) umeonyesha dalili za kupoteza mvuto baada ya kuwavutia idadi ndogo ya wananchi mkoani Rukwa, hususan katika Jimbo la Nkasi Kaskazini.
Tukio hilo lilitokea leo wakati viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Tundu Lissu, walipofika katika eneo hilo kuendelea na kampeni yao. Hata hivyo, mkutano huo uligeuka kuwa kichekesho baada ya waandaaji kugundua kuwa waliojitokeza kwa wingi ni watoto wadogo badala ya wapiga kura wenye sifa. Kutokana na hali hiyo, viongozi wa Chadema walilazimika kuwaimbisha nyimbo za watoto, jambo lililozua mijadala mbalimbali kuhusu mwelekeo wa kampeni hiyo.
Wachambuzi wa siasa wameeleza kuwa hali hii ni ishara kwamba ujumbe wa kampeni ya No Reform No Election haujapata uungwaji mkono unaotarajiwa na chama hicho, hasa katika maeneo ya vijijini ambako chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinaendelea kushika hatamu. Pia, imezua maswali kuhusu mbinu za Chadema katika kuhamasisha wananchi kushiriki mijadala ya kisiasa na kudai mabadiliko wanayoyapigania.
Hali kama hii imekuwa ikijirudia katika mikutano kadhaa ya Chadema, ambapo idadi ya washiriki imekuwa ndogo na mara nyingine mikutano hiyo kuonekana kutowavutia wananchi wa kawaida. Baadhi ya wachambuzi wanasema kuwa hili linatokana na kutokuwa na ajenda inayowagusa moja kwa moja wananchi wa kawaida, huku wengine wakidai kuwa upinzani bado haujaweza kutoa mbadala wa sera unaoeleweka.
Huku CCM ikiendelea kutekeleza Ilani yake kwa vitendo, hali ya Chadema katika kampeni ya No Reform No Election inazidi kuzua maswali kuhusu nafasi yao katika siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi ujao. Ikiwa hali hii itaendelea, kuna uwezekano mkubwa kampeni hiyo ikapoteza mwelekeo zaidi, na hatimaye kufifia kabisa kabla ya kufikia malengo yake.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Uchambuzi wa bajeti kuchochea ufanisi taasisi za umma
Hassani MakeroMar 24, 2025KAMPENI YA 'NO REFORM NO ELECTION' YAPOTEZA MWELEKEO RUKWA
Hassani MakeroMar 24, 2025TAMASHA LA KUOMBEA UCHAGUZI KUFANYIKA MIKOA YOTE TANZANIA
Hassani MakeroMar 24, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment