Wizara ya haki nchini
humo ilisema kundi hilo lilikuwa limesambaza nyaraka zilizokuwa na ujumbe wa
kuchochea chuki dhidi ya makundi mengine.
Mawakili waliokuwa
wanatetea kundi hilo wamekanusha madai hayo na wamesema watakata rufaa.
Kundi hilo la kidini
lina waumini 175,000 nchini urusi, taifa ambalo wafuasi wa madhehebu hayo
waliteswa na kudhulumiwa wakati wa utawala wa Josef Stalin.
Inakadiriwa kwamba kuna
watu milioni nane kote duniani ambao ni waumini wa madhehebu hayo ya Kikristo,
yanayofahamika sana kwa kampeni zake za kwenda nyumba kwa nyumba kutafuta
waumini wapya.
Wafuasi wa kundi hilo la
kidini wanasema hatua ya kuharamisha kundi hilo ina maana kwamba shughuli zake
pia ni haramu kisheria.
Wizara ya haki iliiomba
mahakama kufunga makao makuu ya kitaifa ya kundi hilo la kidini karibu na mji
wa St Petersburg, mashirika ya habari ya Urusi yalisema, pamoja na kupiga
marufuku baadhi ya vitabu vyenye msimamo mkali vinavyochapishwa na kundi hilo.
Moja ya vijitabu
vilivyosambazwa na kundi hilo nchini Urusi vilimnukuu mwandishi mashuhuri wa
vitabu Leo Tolstoy akieleza imani kuu ya kanisa la Orthodox la Urusi kama
ushirikina na uchawi.
Maafisa wamelituhumu
kundi hilo la kidini kwa kuharibu familia, kupanda mbegu za chuki na
kuhatarisha maisha.
Mashahidi wa Yehova
wanasema tuhuma hizo si za kweli.
Msemaji wa kundi hilo
aliambia shirika la habari la AFP kwamba alishangazwa sana na uamuzi huo.
"Sikutarajia kwamba
hilo linaweza kutokea katika Urusi ya sasa, ambapo katiba inawahakikishia raia
uhuru wa kuabudu," alisema Yaroslav Sivulsky.
Kundi la Mashahidi wa
yehova lilianzishwa nchini Marekani karne ya 19.
Huwa wanafasiri Biblia
moja kwa moja na miongoni mwa mengine waumini wake hawaruhusiwi kutoa au
kupokea damu.
Huwa hawatazamwi na
makanisa mengine makuu ya zamani ya Kikristo kama madhehebu makuu.
Wakati wa utawala wa
Joseph Stalin katika Muungano wa Usovieti, kundi hilo lilipigiwa marufuku na
maelfu ya waumini wake wakapelekwa Siberia kuteswa. Makundi mengine ya kidini
yalihangaishwa na serikali pia.
Muungano wa Usovieti
ulipoporomoka, dini za Kikristo zilifufuka Urusi na marufuku dhidi ya Mashahidi
wa yehova ikaondolewa mwaka 1991.
Lakini msimamo wa
serikali dhidi ya kundi hilo la kidini ulianza kuwa mkali tena na mwaka 2004
lilituhumiwa kwa kuwaandikisha watoto kuwa waumini na pia kuwazuia waumini
kupokea usaidizi wa kimatibabu.
No comments:
Post a Comment