Monday, June 29, 2020

RC MAKONDA awanyima USINGIZI WAPINZANI mkoani DAR ES SALAAM!
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ameendelea na ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Miongoni mwa Miradi aliyoikabidhi RC Makonda iliyotekelezwa kupitia Ilani ya CCM kwa upande wa Jimbo la Kinondoni ni Mradi wa Soko la Magomeni lenye thamani ya Shilingi Bilioni 8.9, Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto hospital ya Mwananyamala inayogharimu Bilioni 3 na Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja Cha Mpira Mwenge chenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.5.
Aidha RC Makonda pia amekabidhi Mradi wa Ujenzi Barabara ya Morocco hadi mwenge yenye thamani ya Bilioni 69.7, Mradi wa Kituo cha Mabasi Mwenge Bilioni 2.5 na Kituo cha Afya Kigogo chenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.5.
Kesho Jumatano RC Makonda ataendelea na ziara yake kwenye Jimbo la Kibamba ambapo atakabidhi miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Chama cha Mapinduzi CCM.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
KUTOKA MAGAZETINI JUNI 30, 2020 NDANI NA NJE YA TANZANIA
Older Article
Malawi swears in new president Lazarus Chakwera
Rais Samia ahutubia Baraza la Eid El Fitr Jijini Dar es Salaam
Hassani MakeroMar 31, 2025MWENYEKITI WA CCM MKOA TANGA ASISITIZA AMANI SHEREHE ZA EID ELFITR
Hassani MakeroMar 30, 2025TCB BANK YAENDELEA KUIMARISHA UCHUMI WA MTU MMOJA MMOJA
Hassani MakeroMar 28, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment