Ameongeza kuwa anayo mengi ya kujifunza hasa katika utekelezaji wa miradi ya maji kwa kutumia utaratibu wa ‘Force Account’ ambao unawatumia zaidi watalaam wa ndani badala ya wakandarasi katika utekelezaji wa mradi.
Waziri wa Maji Mhe. Profesa Mbarawa (Mb) anasema tangu kuanza kwa utaratibu huo, matokeo makubwa yameonekana na anawataka wataalam wa Wizara yake kujiandaa kutekeleza miradi mbalimbali kwa mtindo huo.
Prof. Mbarawa anasema baada ya kuanza kutumia utaratibu huo Serikali imeweza kukamilisha miradi kwa haraka zaidi, gharama za utekelezaji wa miradi zimepungua kwa kiasi kikubwa na umesaidia kuondoa migongano baina ya Serikali na wakandarasi.
Ipo mifano michache iliyodhihirika katika ziara hiyo. Mradi wa maji wa Ngogwa-Kitwana ulipangwa kutekelezwa na mkandarasi kwa shilingi bilioni 4.6.
Mradi huo ulioanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Machi 2020 unatarajia kukamilika ndani ya miezi sita jambo ambalo linatajwa na Waziri Prof. Mbarawa kuwa ni muda mfupi sana ukilinganisha na muda ambao wakandarasi wamekuwa wakiutumia kutekeleza miradi ya aina hiyo.
No comments:
Post a Comment