Serikali kupitia Wizara ya
Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeandaa Rasimu ya Muswada wa Sheria itakayoweka bayana taratibu na mfumo wa
usimamizi na udhibiti wa bishara ya
chuma chakavu katika hatua mbalimbali za uzalishaji, ukusanyaji, usambazaji,
uuzaji na uyeyushaji wake kwa kuzingatia uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa manufaa ya Taifa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa
Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge Mjini Dodoma.
Biashara ya Chuma chakavu
imeshamiri hapa nchini na duniani kwa ujumla na hili limetokana na mahitaji ya vyuma chakavu ambapo kumetumiwa na
wahalifu kuaharibu miundombinu
iliyojengwa kwa vyuma kwa nia ya kupata chuma ili waiuze kama chuma chakavuâ€Alisema Mwijage.
Amesema ili kukabiliana na
hujuma hizi Mamlaka husika zikiwemo TANESCO, TANROADS na RAHACO wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na jeshi la
Polisi ikiwemo kutumia walinzi wa
Taasisi husika ili kulinda rasilimali hizo.
Amesisitiza kuwa Muswada
huu umeweka wazi na bayana adhabu itakayotolewa kwa mtu atakayebainika kuharibu miundombinu.
Aidha Mhe.Mwijage ametoa
wito kwa watanzania kutoa taarifa pindi waonapo mtu anayehujumu miundombinu kwa namna yote ile.
“Natoa wito kwa wenye
viwanda na wafanyabiashara wa vyuma chakavu
jiepusheni na ununuzi wa vyuma ambavyo asili yake ina mashaka
na tutaharakisha sheria hii ili kutatua tatizo hili,” aliongeza Mwijage.
No comments:
Post a Comment