Tuesday, June 20, 2017

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Magomeni kizimbani kwa rushwa
Hakimu wa Mahakama ya
Mwanzo Magomeni na mfanyabiashara wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu kujibu mashtaka manne ya kuomba na kupokea rushwa.
Mwendesha Mashtaka kutoka
taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Emmanuel Jacob amewataja washtakiwa
hao kuwa ni Omary Mohammed Abdallah ambaye ni Hakimu na mfanyabiashara
George Joseph Barongo.
Wakisomewa mashtaka yao
mbele ya Hakimu Mkazi Respicious Mwijage, imedaiwa kuwa, kati ya January na
Februari 12/ 2017 hakimu Omary alitenda kosa.
Imedaiwa kuwa, siku hiyo
Omary akiwa muajiriwa wa Mahakama ya Mwanzo Kinondoni aliiomba rushwa ya
sh. 205,000 kutoka kwa Agnes Nyenza kwa ajili ya kumsaidia kwenye kesi yake ya
mirathi ya namba 570/2016 ambayo ilikuwa mbele yake.
Katika shtaka la pili Hakimu
Omary anadaiwa kupokea rushwa ya kiasi hicho cha fedha Kutoka kwa Nyenza ili
aweze kumsaidia katika kesi hiyo.
Mahakama imeendelea
kuambiwa kuwa, kati ya Februari na Machi mwaka huu, jijini Dar es salaam,
Hakimu Omary akiwa na mfanyabiashara Barongo waliomba rushwa ya sh. Milioni
moja kutoka kwa Nyenza kwa ajili ya kumsaidia katika kesi hiyo ya mirathi.
Wakili wa Takukuru
aliendelea kuieleza mahakama kuwa, siku na mahali hapo watuhumiwa hao wote kwa
pamoja walipokea rushwa ya sh. 500,000 kwa ajili ya kumsaidia Agnes Nyenza
kwenye kesi yake ya mirathi ambayo iko mbele ya hakimu huyo Omary Mohammed wa
Mahakama ya Mwanzo Magomeni.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
VIGOGO WA ESCROW NA IPTL WAPANDISHWA KIZIMBANI JANA
Older Article
WADAIWA KODI YA MAJENGO KUBURUZWA MAHAKAMANI
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment