Friday, February 15, 2019

BENKI YA NBC YACHANGIA UJENZI WA KITUO CHA POLISI RUANGWA MKOANI LINDI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (wa pili kushoto), mara baada ya kupokea msaada wa mifuko 1000 ya saruji kutoka NBC, kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi. Wengine kutoka kushoto ni, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, Neema Singo, Meneja Mahusiano, William Kallaghe, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Flora Molel na Mkurugenzi wa Kitengo cha Malalamiko, Sarah Laiser.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (wa pili kushoto), akipokea mfano wa hundi ya shs 11,270,000 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, kwa ajili ya kununulia mifuko 1000 ya saruji kama mchango wa NBC kuchangia ujenzi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Ruangwa, Mkoani Lindi. Hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
BENKI ya NBC imetoa msaada wa mifuko 1000 ya saruji
kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuchangia ujenzi
wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.
Msaada huo umekabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa
NBC, Theobald Sabi kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika ofisi zake Ikulu jijini
Dar es Salaam leo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji
wa NBC, Theobald Sabi anasema NBC ni Benki
ya Wazalendo na tunajiona fahari kuweka juhudi zetu katika kuhakikisha kila mwananchi
na mzalendo waTaifa letu anaishi kwa usalama na utulivu.
“Kama taasisi ya fedha ni imani yetu kuwa Jeshi
la Polisi likiwezeshwa kwa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo majengo ya vituo pamoja
na makazi ya askari litaweza kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi ambayo
ni kulinda usalama wa raia na mali zao.
Benki ya NBC inajua pia eneo litakalojengwa kituo
hiki wapo wateja wetu na wale wateja watarajiwa hivyo ujenzi wa kituo hiki utasaidia
sana kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika wilaya hiyo hivyo kuwafanya wakazi
wake kuzalisha mali katika hali ya utulivu hiyvo kukuza uchumi wao na wa Taifa.
“Benki ya NBC inapenda kutoa pongezi kwa Serikali
ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli kwa jitihada zake katika
kujenga mazingira wezeshi kwa sekta binafsi ili kwa pamoja kutimiza azma ya kuelekea
Tanzania ya viwanda.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Uber yazindua bima ya Ulinzi dhidi ya Majeraha kwa madereva na abiria nchini Tanzania bila gharama yoyote ya ziada
Older Article
At last, the boys secured their inheritance rights
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment