Tuesday, June 30, 2020

Home
KITAIFA
RC MAKONDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TBA KUKAMILISHA UJENZI WA JENGO LA MANISPAA YA UBUNGO, AGOMA KUKABIDHI MRADI HUO KWA CCM
RC MAKONDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TBA KUKAMILISHA UJENZI WA JENGO LA MANISPAA YA UBUNGO, AGOMA KUKABIDHI MRADI HUO KWA CCM
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wakazi wa jimbo la Kibamba wakakati akikabidhi mradi wa standi mpya ya kisasa ya mabasi inayojengwa mbezi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wakazi wa jimbo la Kibamba wakakati akikabidhi mradi wa standi mpya ya kisasa ya mabasi inayojengwa mbezi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kisare Makori akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Mkurugenzi wa Manspaa ya Ubungo Beatrice Dominic akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Mwenyekiti wa chama Wilaya ya Ubungo Ndg.Lucas Mgonja akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Maulid Mtulia mwenye tisheti ya njano katikati akipiga kwata pamoja na vijana wa hamasa wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipotembelea na kukabidhi kituo cha afya kilichopo Kimara mwisho
Mkuu wa Mkoa akipiga kwata na vijana wa hamasa Picha zote na Brian Peter
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amegoma kukabidhi kwa Chama cha Mapinduzi CCM Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Manispaa ya Ubungo kutokana na ujenzi huo kusuasua hadi sasa ambapo amemtaka Mkandarasi wa ujenzi huo Wakala wa Ujenzi TBA kuhakikisha anakabidhi mradi ndani ya mwezi mmoja kuanzia Leo.
RC Makonda amechukizwa kuona ujenzi huo ulitakiwa kukamilika na kukabidhiwa Mwezi Disemba mwaka jana lakini mkandarasi aliomba kuongezewa miezi sita lakini hadi sasa Ujenzi haujakamilika jambo lonaloendelea kuwafanya Watumishi wa Manispaa hiyo kufanya kazi katika mazingira magumu.
Hayo yamejiri wakati wa Mwendelezo wa Ziara ya RC Makonda kukabidhi miradi kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambapo kwa siku ya leo amekabidhi miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 196.4 kwa upande wa Jimbo la Kibamba.
Miongoni mwa miradi aliyokabidhi RC Makonda ni Stand ya Mabasi ya Mikoani ya Mbezi Luis inayogharimu Bilioni 50, Upanuzi wa Barabara ya Kimara hadi Kibaha yenye urefu wa Km 19.2 na gharama ya Bilioni 140.4, Upanuzi wa Mtambo wa Maji Ruvu Juu na ujenzi wa Tank Kibamba wa thamani ya Milioni 624.
Aidha RC Makonda pia amekabidhi mradi wa Ujenzi wa Mabanda Saba ya Wafanyabiashara Mbezi Luis unaogharimu Bilioni 1.5 na Ujenzi wa Kituo cha Afya Kimara Bilioni 1.5.
Ziara ya RC Makonda itaendelea siku ya kesho kwenye Jimbo la Ubungo ambapo atakabidhi miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
TANZANIA YAINGIA KUNDI LA NCHI ZA KIPATO CHA KATI
Older Article
JESHI LA POLISI LABAINI CHANZO CHA AJALI YA BASI LA PRESDAA, LAFUTA LESENI YA DEREVA
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment