RC MAKONDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TBA KUKAMILISHA UJENZI WA JENGO LA MANISPAA YA UBUNGO, AGOMA KUKABIDHI MRADI HUO KWA CCM - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Tuesday, June 30, 2020

demo-image

RC MAKONDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TBA KUKAMILISHA UJENZI WA JENGO LA MANISPAA YA UBUNGO, AGOMA KUKABIDHI MRADI HUO KWA CCM


IMG_6395
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wakazi wa jimbo la Kibamba wakakati akikabidhi mradi wa standi mpya ya kisasa ya mabasi inayojengwa mbezi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
IMG_6593
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wakazi wa jimbo la Kibamba wakakati akikabidhi mradi wa standi mpya ya kisasa ya mabasi inayojengwa mbezi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
IMG_6349
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kisare Makori  akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
IMG_6662
Mkurugenzi wa Manspaa ya Ubungo Beatrice Dominic akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
IMG_6232
Mwenyekiti wa chama Wilaya ya Ubungo Ndg.Lucas Mgonja akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.
IMG_6647
Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Maulid Mtulia  mwenye tisheti ya njano katikati akipiga kwata pamoja na vijana wa hamasa wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipotembelea na kukabidhi kituo cha afya kilichopo Kimara mwisho
IMG_6660
Mkuu wa Mkoa akipiga kwata na vijana wa hamasa Picha zote na Brian Peter

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amegoma kukabidhi kwa Chama cha Mapinduzi CCM Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Manispaa ya Ubungo kutokana na ujenzi huo kusuasua hadi sasa ambapo amemtaka Mkandarasi wa ujenzi huo Wakala wa Ujenzi TBA kuhakikisha anakabidhi mradi ndani ya mwezi mmoja kuanzia Leo.

RC Makonda amechukizwa kuona ujenzi huo ulitakiwa kukamilika na kukabidhiwa Mwezi Disemba mwaka jana lakini mkandarasi aliomba kuongezewa miezi sita lakini hadi sasa Ujenzi haujakamilika jambo lonaloendelea kuwafanya Watumishi wa Manispaa hiyo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Hayo yamejiri wakati wa Mwendelezo wa Ziara ya RC Makonda kukabidhi miradi kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambapo kwa siku ya leo amekabidhi miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 196.4 kwa upande wa Jimbo la Kibamba.

Miongoni mwa miradi aliyokabidhi RC Makonda ni Stand ya Mabasi ya Mikoani ya Mbezi Luis inayogharimu Bilioni 50, Upanuzi wa Barabara ya Kimara hadi Kibaha yenye urefu wa Km 19.2 na gharama ya Bilioni 140.4, Upanuzi wa Mtambo wa Maji Ruvu Juu na ujenzi wa Tank Kibamba wa thamani ya Milioni 624.

Aidha RC Makonda pia amekabidhi mradi wa Ujenzi wa Mabanda Saba ya Wafanyabiashara Mbezi Luis unaogharimu Bilioni 1.5 na Ujenzi wa Kituo cha Afya Kimara Bilioni 1.5.

Ziara ya RC Makonda itaendelea siku ya kesho kwenye Jimbo la Ubungo ambapo atakabidhi miradi mbalimbali ya Maendeleo.

 HABARI KATIKA PICHA

IMG_6208

IMG_6231

IMG_6253

IMG_6328

IMG_6336

IMG_6350

IMG_6393

IMG_6414

IMG_6439

IMG_6454

IMG_6554

IMG_6556

IMG_6557

IMG_6569

IMG_6621

IMG_6637

IMG_6330

IMG_6393+-+Copy

IMG_6397+-+Copy

IMG_6522

IMG_6617+-+Copy

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages

Contact Form

Name

Email *

Message *