WENYE VIWANDA WAPEWA ELIMU YA MATUMIZI BORA YA NISHATI YA UMEME - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Wednesday, July 8, 2020

WENYE VIWANDA WAPEWA ELIMU YA MATUMIZI BORA YA NISHATI YA UMEME


Wamiliki wa Viwanda Wilaya za Dodoma na Bahi wametakiwa kuwa na utamaduni wa kufanya ukarabati wa mara kwa mara na kubadili vifaa vilivyo tumika kwa muda mrefu ili kuepuka gharama zisizo za lazima na matumizi makubwa ya nishati ya umeme.

Wito huo umetolewa na Mhandisi mtafiti wa Tanesco, Aurea Bigirwamungu wakati wa kutoa elimu juu ya matumizi bora ya Nishati ya Umeme katika wilaya za Dodoma na Bahi.

Bigirwamungu ameshauri wamiliki hao kuwa na utamaduni wa kubadilisha mota za kuendeshea mitambo yao katika uzalishaji ili kutumia nishati ya umeme inayoendana na gharama ya matumizi sahihi ya nishati hiyo.

Naye Ofisa Tawala wa Kampuni ya Nyanza Road Workers, Bakari Mugini ameishukuru Tanesco kwa  mafunzo yaliyofanya kujua namna ya matumizi sahihi ya nishati hiyo.

Mugini ameeleza kuwa katika mafunzo hayo wamepata elimu juu ya usalama wa miundombinu iliyopo katika viwanda ili kuongeza uzalishaji wa bidhaa zao.

"Haya ni mafunzo muhimu Sana kwenu kwani yametufanya kujua masuala ya usalama wa miundombinu iliyopo viwandani" alisema Mugini.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages