Thursday, May 16, 2024

Home
BIASHARA
Serikali kuendelea kushirikiana na Benk ya Absa kuendeleza nguvu kazi ya Taifa - Katambi
Serikali kuendelea kushirikiana na Benk ya Absa kuendeleza nguvu kazi ya Taifa - Katambi
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imesema itaendelea kushirikiana na uongozi wa Benki ya Absa nchini katika Programu ya Leaders in the Making "viongozi wa kesho". Program hiyo inalenga kuendeleza nguvukazi ya taifa hususani vijana kwa manufaa ya Benki hiyo na Taifa kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakati wa mahafali ya wahitimu waliofuzu katika Programu ya Leaders in the Making "viongozi wa kesho" leo tarehe 14 Mei 2024.
Mhe.Katambi amefafanua kuwa Programu hiyo inaunga mkono jitahada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Serikali ya Awamu ya Sita katika Kukuza Ujuzi ambapo mafunzo imekuwa ikitoa mafunzo kwa wafanyakazi na watafuta kazi ili kukuza na kuendeleza ujuzi walionao.
Ameongeza kuwa Serikali inaitambua Programu hiyo kwa mchango wake mkubwa kwenye maendeleo ya nguvu kazi ya taifa na maendeleo ya taifa kwa ujumla hasa ukizingatia mazingira ya kazi yanabadilika haraka ambapo yanahitaji wahitimu kujiongezea ujuzi na uwezo wao zaidi.
Aidha; Mhe. Katambi ameyataka Mashirika mengine kuiga mfano wa Absa na kuzindua miradi kama hiyo kwa kujitegemea au kwa ushirikiano, kwani jukumu la kuwapa wahitimu ujuzi unaokidhi mahitaji ya kazi na ajira ni jukumu kubwa ambalo haliwezi kufanywa na Shirika moja peke yake au Serikali peke yake.
Awali akiongea katika Mahafali hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa, Bw. Obedi Laiser, amesema Programu hiyo ya ushiriki wa wahitimu inaendana na lengo kuu la benki ya Absa, ambalo ni Kuiwezesha Afrika na Tanzania yenye viongozi bora wa sasa na baadae.
Naibu Waziri Ofisi za Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Mhe. Patrobasi Katamb (wa pili kushoto), akikabidhi tuzo kwa mmoja wa wahitimu wa program ya Leaders in the Making ‘Viongozi wa Kesho’ iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na Kampuni ya Empower, Bi. Shanira Msale katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni, Mkurugenzi Mwenza wa Empower, Bi. Miranda Naiman, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Obedi Laiser na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa, Bwana Patrick Foya.
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
CRDB Insurance Na ACRE Africa Washirikiana Kuboresha Bima Ya Mifugo
Older Article
Absa Dar City Marathon 2024 donates hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital
AKIBA COMMERCIAL BANK PLC YATOA ELIMU YA KIFEDHA KWA WATEJA WAKE KARIAKOO
kilole mzeeApr 13, 2025WADAU ZAIDI YA 500 KUSHIRIKI WIKI YA AZAKI 2025 MWEZI JULAI ARUSHA
Hassani MakeroApr 11, 2025JUBILEE HEALTH INSURANCE YAJIVUNIA MAFANIKIO YAKE,YAPEWA TUZO YA TSEA 2025
Hassani MakeroApr 08, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment